LATEST POSTS

Thursday, August 20, 2015

KUNDI LA KWANZA LA WANAMUZIKI KUPATA BIMA YA AFYA KESHO,ASEMA JOHN KITIME.



                                                         BIMA YA AFYA  

Kundi  wanza la wanamuziki waliojiandikisha kujiunga katika mpango wa Bima ya afya,linatarajiwa kuanza kupata huduma  hiyo rasmi kesho Tarehe 21 August 2015 katika ofisi ya BASATA Jijini Dar-Es Salaam ambapo watapatiwa Kadi zitakazowawezesha kupata huduma ya matibabu katika Hospitali zote kubwa za Serikali na baadhi za Binafsi kama vile Regency nk.
 
                      NDUGU JOHN KITIME;Kiongozi wa Mtandao wa Muziki Nchini.

 Akiongea na Kavasha,Kiongozi wa Mtandao wa Muziki Nchini Anko John Kitime amesema kuwa  mpango huo umeratibiwa na Mtandao wa Muziki nchini kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Nchini NHIF na kwamba Mwanamuziki atalazimika kutoa kiasi cha Tshs 96800/= ambayo itamuwezesha kupata huduma hiyo kwa mwaka mzima .

 
                ANKO JOHN KITIME''Wanamuziki tujitokeze kwa wingi kwa ajili ya afya zetu''.

Anko Kitime ameongeza kuwa kiasi hicho ni kidogo kulinganisha na gharama halisi ya matibabu ambayo hayana dhamana yoyote ile,amewashauri viongozi wa vikundi vya muziki na wanamuziki wenyewe kujitokeza kwa wingi ili kupata huduma hiyo.


               
                      NDUGU FRESH JUMBE''Kama itaruhusu kuchukua dawa katika maduka 
                                                    ya madawa itakua nzuri sana''.

 Amesema kuwa Mtandao anaouongoza umefanya juhudi kubwa kuunganisha Mfuko huo wa Bima na Wanamuziki ili kujaribu kusaidia wanamuziki hao pale wanapofikwa na maradhi kwani huwa katika wakati mgumu kutokana na baadhi yao  kutomudu gharama za matibabu pale wanapokuwa hawawezi kufanya shughuli yao hiyo.

                                  
                             Venance Geuza(Anko Vena)''Ni fursa nzuri ambayo tuliitafuta kwengine''.

Wakiongea na KAVASHA kwa nyakati tofauti,Baadhi ya wanamuziki wamesifu mpango huo na kusema umekuja wakati ukihitajika,wanamuziki hao ni Musa Karenga, Fresh Jumbe,Elibariki Kunukula na Venance Geuza ambae alisema ni mpango mzuri na viongozi wahakikishe umefanikiwa kwani wapo wengine walitoka katika muziki na kwenda kuajiriwa kwenye sekta rasmi ili kupata huduma hiyo ya Bima ya Afya.
KAVASHA inawatakia kazi njema  na kuwaomba mjitokeze kwa wingi kupata huduma hiyo muhimu na adhimu.

0 comments:

Post a Comment