LATEST POSTS

Monday, September 21, 2015

MARTIN KIBOSHO;UVUMILIVU NA KUJITUMA NDIO KILA KITU KATIKA MUZIKI,SEHEMU YA 1.


        SAFARI YA KIMUZIKI YA MARTIN KIBOSHO.


Mwenyewe anasema;

                                               Martin Kibosho akiwa kazini.

Nilianza muziki Mwaka 2000,nilianza na Mand inaitwa Muungano nilikua kama drummer chipukizi nilikua na mpiga drums maarufu anaitwa kang’ombe kwa sasa yuko Msondo Ngoma Music nilikaanae kwa muda wa miezi 6 akiwa ananionyesha vitu fulani,baada ya hapo nikatoka kwenda African Beats kwa mzee Mafumu Bilali nilikaa mwaka 1 nikatoka nilipita viband vingi sana vidogovidogo wakati mwingine na mdogo wangu James Kibosho ila yeye alidumu sana na Bendi ya The African Stars''Twanga Pepeta''kabla ya kutoka hivi karibuni.

 

                                       Vipaji Band Jukwaani Nchini Ufaransa.

Viband nilivyopita baada ya hapo ni Tango Stars,Wasi Musica,Nina musica,Santon Band, Zote nilikua napitapita tu ili nipate ujuzi zaidi kitu nilichofanikiwa hadi kufikia Bendi zilikoa kubwa nchini kama Twanga Chipolopolo nilipiga album yote ya ''hujafa hujasifiwa''na Extra Bongo 3x3 na Mtenda akitendewa,African Revolution''wana TamTam''Mchinga Sound''wana TimbaTimba'' chini ya Ally Choky tukarekodi albam ya''Mwaka wa Tabu'' zikafatia safari za Dubai na Muscut kupiga kwa mkataba miziki ya kopi na hatimae kwenye Band hii niliyonayo huku Australia ambayo tunapiga mizki mbalimbali ya kiafrika na Dunia kwa ujumla ikiwepo ya kusindikiza michezo ya sarakasi nk

                             Kundi la wanasarakasi wanaoshirikiana na Vipaji Band. 
Band  hii  inaitwa Vipaji ambapo kuna wanamuziki  kama Martin Kibosho,Kado Bass,Moses  Mpiga Saxophone,Kuna Dr  Kumpeneka anaimba na kupiga percussion kuna Maneno Uvuruge mpiga guitar, kuna Tom Nigura mpiga keyboard  na wa mwisho ni kiongozi wetu Bob Rudala nadhani ni majina maarufu katika tasnia ya muziki wa dansi nchini Tanzania,Pia kuna mwimbaji wa kike kutoka zimbabwe anaitwa Seletemba .

                                                                 Vipaji Band.
 Tumezunguka na Vipaji Band sehemu mbalimbali Duniani na kwa sasa napenda wasomaji wetu uwawekee show yetu ya nchini Ufaransa ambayo ni moja ya Tour ndefu na yenye mafanikio makubwa.


                             Foleni ya kuingia kwenye show ya Vipaji Band Jijini Paris.
 Hiyo Show tulifanya Ufaransa Mjini Paris,ni show kubwa sana hapo kuna mataifa manne, tuko sisi watu wa Band wote ni watanzania kuna group kutoka Ethiopia,Zimbabwe na South Africa,hapo sisi kazi yetu ni kupiga music laini, tunapiga muziki tofauti style zote kiafrika ndio sana kizungu kidogo coz hiyo ni show ya kiafrika

Ilikua mwaka jana ambapo  tulifanya show mjini Paris mwezi mmoja baadae  tukaanza  tour ya mikoani tulizunguka Miji 22 Nchini Ufaransakwa u jumla wake ambapo ilitufikisha mpaka Uswisi  jumla tulikaa miezi mitatu.


              Kiongozi wa Kundi hilo Bob Rudala akiwa na wacheza Sarakasi wa kundi hilo.
 
Dr.Kumpeneka,Maneno Uvuruge,Martin Kibosho,Moses Saxophone,Tom Keyboard,Kiongozi Bob Rudala na Kado Bass.



Tuangalie picha mbalimbali kuona yale yaliyojiri katika ziara hiyo ya Ufaransa,Tour de France;



                                                   Paris,France.

 
                                                      Paris,France.

 
                                                        Paris,France.

                                                    Paris,France.

                        
                                                    Paris,France.

                                                            France.
                                                  France.

 
                                                      France.

                       
                                                  France.
                                             France.

 
                                             In France.
 
                                                 France.
           
                                              Kado Bass akiwajibika.

 
                                                 France.
 
                    Martin akiwa na wapiga ngoma Mjini Paris Ufaransa.

 
                                            France

 
                                                      France.

                      
                                                       France.

            
                                              Martin Mzigoni.
 
                                                France.

3 comments:

  1. Safi sana martin kibosho,siku zote ukiwa na uvumilivu bidii na heshima pamoja na kujituma lazima ufike mbali. Miziki haitaki kuridhika.
    Gig up vipaji band
    Big up Bob Rudala, wewe ndio mwanzilishi wa vipaji band unajituma sana.

    ReplyDelete
  2. Safi sana martin kibosho,siku zote ukiwa na uvumilivu bidii na heshima pamoja na kujituma lazima ufike mbali. Miziki haitaki kuridhika.
    Gig up vipaji band
    Big up Bob Rudala, wewe ndio mwanzilishi wa vipaji band unajituma sana.

    ReplyDelete